Tuesday, March 31, 2009

Maisha Furaha - Maarifa Ya Kuanda Mishkaki Asili

Mahitaji

  1. Nyama nusu kilo 
  2. Papai mbichi 
  3. Tangawizi mbichi 
  4. Limao 2 
  5. Ndizi 3
  6. Chumvi kiasi 

Kuandaa

  1. Katakata nyama vipande vidogo,nyama iwe nundu tafadhali 
  2. Ponda tangawizi weka kwenye nyama 
  3. Kamulia malimao 
  4. Fefenya chumvi 
  5. Katakata papai na weka kwenye nyama 
  6. Vichanganye na vifunike viache kwa nusu saa 
  7. Washa moto kama unatumia mkaa
  8. Chomeka nyama kwenye chuma au stick(zipo special kwenye supermarkets) 
  9. Anza kuchoma hadi ziwe ukaa
  10. Menya ndizi na ziweke motoni zigeuze zikiiva utaona zimekuwa ngumu 
  11. Andaa sahani weka mishkaki yako na ndizi na matango/pilipili au kashumbari kama unapenda 

 Maisha Furaha!

No comments: